Numbers 33:1-6
Vituo Katika Safari Ya Waisraeli
1 aHivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Musa na Haruni. 2 bKwa agizo la Bwana, Musa aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao: 3 cWaisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote, 4 dwaliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.5 eWaisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 fWakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
Copyright information for
SwhKC