Numbers 33:1-6

Vituo Katika Safari Ya Waisraeli

1 aHivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Musa na Haruni. 2 bKwa agizo la Bwana, Musa aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:

3 cWaisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote, 4 dwaliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 eWaisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 fWakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
Copyright information for SwhKC